Mpanda FM

Serikali ya mtaa Mpanda hotel yaridhishwa na ujenzi wa choo

15 January 2026, 2:55 pm

Uongozi wa shule ya msingi Mpanda pamoja na mwenyekiti wa mtaa. Picha na Roda Elias

“Tumeridhisha na ujenzi wa choo”

Na Roda Elias

Serikali ya mtaa wa Mpanda hotel  manispaa ya Mpanda mkoani Katavi imeridhishwa na ujenzi wa mradi wa  matundu ya choo cha wasichana unaoendelea  katika shule ya msingi Mpanda.

Akizungumza katika ukaguzi wa mradi huo uliofanyika katika shule ya msingi Mpanda mwenyekiti wa mtaa huo Ibrahim Msanda amempongeza mwalimu mkuu wa shule hiyo kwa kusimamia ujenzi wa choo hicho.

Sauti ya mwenyekiti

Choo cha wasichana katik shule ya msingi Mpanda

Kwa upande wao wazee wa baraza la mtaa huo wakiongozwa na mzee Robert Mgangala  wameupongeza uongozi wa shule hiyo  huku wakiomba kupatikana kwa ufumbuzi juu ya changamoto Mbalimbali zinazoikumba shule hiyo.

Sauti ya wajumbe

Akitoa taarifa ya mradi huo mwalimu mkuu wa shule hiyo Khadija Chikawe amesema kuwa wamepitia changamoto kutoka kwa mzabuni ambapo mpaka sasa wamepata ufumbuzi wa changamoto hiyo.

Sauti ya mkuu wa shule

Mradi wa ujenzi wa choo cha wasichana  katika shule hiyo  ni mradi ambao umejengwa na serikali na mapato ya ndani ya halmashauri na vyoo hivi vina  matundu saba moja likiwa ni tundu kwa ajiri ya wanafunzi walio na mahitaji maalumu.