Mpanda FM

Maadili ya vijana wa sasa ni tofauti na zamani?

11 December 2025, 12:46 pm

Picha na mtandao

“Watoto wa sasa hivi hawawasikilizi wazazi wao”

Na Janeth Kaombwe

Katika kuadhimisha siku ya haki na maadili kitaifa inayofanyika tarehe 10 mwezi wa 12 kila mwaka, vijana wamehimizwa kuendelea kufuata maadili ya kitanzania kwani kumekuwa na mmomonyoko  wa maadili kwa vijana  Tanzania.

Wakizungumza na Mpanda radio FM baadhi ya wazee mkoani katavi wamesema kuwa maadili ya sasa ni tofauti na ya zamani kwani vijana wengi hawafuati maelekezo wanayopewa na wazazi wao  wala kujituma katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Sauti za wazee

Kwa upande wa baadhi ya vijana wa manispaa ya  Mpanda wamekiri kuwepo kwa  mmomonyoko wa maadili unaosababishwa na vijana wengi kukosa heshima na mwitikio mzuri kutoka kwa wazazi wanapowatuma kufanya vitu mbalimbali .

Sauti za vijana