Mpanda FM

Shumbi “Vijana kuweni na nidhamu ya fedha”

8 December 2025, 3:03 pm

Afisa maendeleo mkoa wa Katavi Anna Shumbi. Picha na Anna Mhina

“Kukamilisha malengo kwanza unatakiwa uwe na msimamo”

Na Leah Kamala

Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametoa maoni yao kuhusiana na umuhimu wakujiwekea malengo ili kuboresha maisha yao binafsi.

Wakizungumza na Mpanda radio FM wananchi hao wamesema kuwa kujiwekea malengo ni hatua muhimu inayoweza kumsaidia mtu kupiga hatua katika maisha na kumuwezesha kufanikisha jambo fulani.

Sauti za wananchi

Nae Afisa maendeleo mkoa wa Katavi Anna Shumbi amesema kuwa kuweka malengo kunawasaidia vijana wengi kujiepusha na matumizi mabaya ya fedha hivyo amewasihi vijana kujiwekea malengo.

Sauti ya afisa maendeleo

Ameongeza kuwa kutojiwekea malengo kunawafanya wananchi kushindwa kupanga matumizi yao na kukosa mwelekeo wa kiuchumi.

Sauti ya afisa maendeleo