Mpanda FM

Viongozi wa dini Katavi watoa tamko la amani

6 December 2025, 12:32 pm

Baadhi ya viongozi wa dini katikati ni padri Katagwa. Picha na Restuta Nyondo

“Sisi kama viongozi wa dini tutashirikiana na wananchi katika kudumisha amani”

Na Restuta Nyondo

Viongozi wa dini mkoani Katavi wametoa tamko la amani na kuhamasisha utulivu na ushirikiano kwa wananchi huku wakisema ni wajibu wa kila mtu kulinda amani na usalama wa nchi.

Tamko hilo limesomwa na padri  James  Katagwa mwenyekiti wa jumuia ya maridhiano  na Amani wilaya ya Mpanda amesema kuwa wao kama viongozi wa dini wapo tayari kwenda kuitangaza imani na kushirikiana na waumini katika kulinda amani.

Sauti ya kiongozi wa dini

Awali akifungua kikao hicho mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko amewaomba viongozi hao katika mafundisho yao kuendelea kuwaasa wazazi  na walezi juu ya malezi yenye maadili kwa vijana wao.

Sauti ya mkuu wa mkoa

Aidha amesema kuwa viongozi wa dini ni tanuru la amani kwa wananchi, na kuwataka kuendelea kutumia njia ya mazungumzo na ushauri ili kuleta maendeleo.