Mpanda FM

Vyanzo vya maji vyasaidia kuzalisha umeme Mpanda

27 November 2025, 11:58 am

Moja ya vyanzo vya maji. Picha na Leah Kamala

“Tunaihamasisha jamii itunze vyanzo vya maji kwa sababu ni muhimu”

Na Leah Kamala

Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameeleza  madhara  katika mazingira endapo  vyanzo vya maji vitaharibiwa.

Wakizungumza na Mpanda radio FM wananchi hao wamesema kuwa madhara hayo yanaweza kusababisha kupungua kwa uzalishaji wa umeme pamoja na kuongezeka kwa magonjwa hivyo wameiomba serikali iendelee kutoa elimu ili kuepukana na madhara hayo.

Sauti za wananchi

Naye Afisa Mazingira Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi Zaituni Rashid amewaelezea wananchi juu ya umuhimu wa kuhifadhi vyanzo vya maji ili kuhakikisha upatikanaji wa maji safi pamoja na kudumisha mazingira na ustawi wa viumbe hai

Sauti ya afisa mazingira

Ni muhimu kwa jamii, serikali na taasisi mbalimbali kushirikiana kulinda vyanzo vya maji kwa ajili ya uzalishaji wa chakula na kuhifadhi mazingira