Mpanda FM

Ukosefu elimu ya uzazi wa mpango chanzo mimba zisizotarajiwa

27 November 2025, 9:26 am

Mtaalam wa afya ya mama na mtoto Katavi Mercy Hezekia. Picha na Anna Mhina

”  Elimu haijitoshelezi inawafikia wazazi wa kike pekee”

Na Anna Mhina

Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameiomba serikali kutoa elimu ya masuala ya uzazi wa mpango ili waweze kuepukana na mimba zisizotarajiwa.

Wakizungumza na Mpanda radio FM wananchi hao wamesema kuwa wanapewa dawa za uzazi wa mpango bila kupewa elimu ya kutosha hali inayopelekea kupata maudhi huku wanaume wakidai kuwa elimu hii inawafikia wanawake pekee.

Sauti za wananchi

Kwa upande wake mtaalam wa afya na kaimu mratibu wa mama na mtoto mkoa wa Katavi Mercy Hezekia  ameeleza hatua zitakazosaidia vijana kuepuka mimba zisizotarajiwa ikiwemo kutoa elimu ya afya ya uzazi wa mpango pamoja na kuelimisha kuhusu njia za uzazi wa mpango.

Sauti ya mtaalamu

Hata hivyo elimu inahitajika zaidi katika kufuta dhana potofu kuhusu uzazi wa mpango huku wanaume wahamasishwe kushiriki katika maamuzi ya uzazi wa mpango ili kupunguza mzigo wa kumuachia mwanamke pekee.