Mpanda FM

Mbarawa akagua ujenzi wa meli nne bandari ya Karema

22 November 2025, 10:31 am

Waziri Mbarawa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa bandari hiyo. Picha na Samwel Mbugi

“Sasa tunajenga meli nne kwa mpigo”

Na Samwel Mbugi

Waziri wa uchukuzi Makame Mbarawa amelizishwa na utengenezaji wa meli nne zinazotengenezwa bandari ya Karema mkoani Katavi.

Akizungumza Mara baada ya ukaguzi amesema kukamilika kwa meli hizo kutochochea uchumi mkoa wa Katavi na kila meli itakuwa na uwezo wa kubeba tani elfu mbili.

Sauti ya waziri Mbarawa

Pia ametoa wito kwa wananchi watakaopata ajila ya kufanya kazi katika bandari hiyo kuwa waaminifu kwa kusimamia usalama vya vyombo na mizigo katika bandari hiyo.

Sauti ya waziri Mbarawa

Kwa upande wake Edward Mabula meneja wa Bandari  ziwa Tanganyika amesema kati ya meli hizo nne moja imekamilika kwa asilimia 90% na ipo tayari kwa majaribio.

Sauti ya meneja wa bandari

Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph aliyemwakilisha mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko amesema kukamilika kwa meli hizo kunaenda kuufungua mkoa wa Katavi kiuchumi.