Mpanda FM

Anyulumye: Vikao vya familia husaidia kutatua migogoro

18 November 2025, 6:59 pm

Afisa ustawi manispaa ya mpanda Anyulumye Longo. Picha na Leah Kamala

“Vikao vinasaidia kusuluhisha migogoro”

Na Leah Kamala

Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameitaka jamii kujenga mazoea ya kukaa na kuzungumza katika vikao  vya  familia.

Wakizungumza na mpanda radio FM wananchi hao wameeleza kuwa vikao vya familia ni msingi muhimu wa kudumisha umoja, kuelekezana, pamoja na kutatua changamoto zinazoikabili familia ili kuimarisha mahusiano ya kifamilia.

Sauti za wananchi

Nae afisa ustawi manispaa ya mpanda mkoani Katavi, Anyulumye Longo amesema kuwa vikao vya familia ni nguzo kuu za ustawi wa jamii kwani husaidia kujenga maadili na kutatua migogoro iliyopo kwenye familia.

Sauti ya afisa ustawi

Longo ameongeza kuwa endapo familia zitashindwa kufanya vikao huweza kupelekea mipango mingi ya familia kushindwa kutekelezeka.

Sauti ya afisa ustawi