Mpanda FM

Jukwaa la wadau wa alizeti laanzishwa Katavi

17 November 2025, 12:59 pm

Picha ya pamoja ya wadau wa jukwaa la zao la alizeti. Picha na Restuta Nyondo

“Lengo ni kutoa fursa kwa ajili kuongeza uzalishaji wa mafuta ya alizeti”

Na Restuta Nyondo

Kuanzishwa kwa jukwaa la wadau wa zao la alizeti mkoani Katavi kunatajwa kama mwanzo wa utatuzi wa uhakika kwa baadhi ya changamoto zinazokabili kilimo cha zao hilo.

Akizungumza na Mpanda Radio Fm mwenyekiti wa chama cha wasindika mafuta ya alizeti Tanzania (TASUPA) na mratibu wa majukwaa ya wadau wa zao la alizeti bw. Ringo Iringo amesema kuwa majukwaa hayo ni daraja kati ya wadau wa zao hilo  na serikali kutambua fursa na changamoto ya uzalishaji wa zao hilo katika kuongeza mnyonyoro wa thamani.

Sauti ya mwenyekiti TASUPA

Jukwaa hilo linajumisha wakulima, wachakataji, wasindikaji ,wauzaji wa pembejeo,serikali na wadau mbalimbali wanaeleza kuwa jukwaa hilo litakwenda kuwasaidia katika kupata elimu zaidi ya kilimo hicho na namna ya kupata masoko ya zao hilo.

Sauti za wanajukwaa

Frank Kaminyoge ni meneja miradi mkoa wa Katavi kutoka shirika la Rikolto amesema kuwa kupitia mradi wa kuongeza mnyonyoro wa thamani katika zao la alizeti amesema kuwa zao hilo bado linakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa teknolojia bora za uzalishaji na uchakataji.

Sauti ya meneja miradi Katavi

Mpaka sasa Tanzania ina jumla ya majukwaa ya wadau wa zao la alizeti 12 katika mikoa 12  ya Tanzania.