Mpanda FM

TAKUKURU Mpanda yaeleza athari za rushwa kipindi cha uchaguzi

22 October 2025, 12:45 pm

Afisa wa TAKUKURU Leonard Minja akizungumza na Mpanda radio. Picha na Anna Mhina

“Rushwa ikifumbiwa macho hupelekea jamii nzima kuathirika”

Na Samwel Mbugi

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi imeweka bayana athari zitokanazo na rushwa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Hayo yamesemwa na afisa wa TAKUKURU Leonard Minja akizungumza na Mpanda radio FM ambapo amesema kama itatokea wakachaguliwa wagombea wanaotokana na rushwa jamii haitaweza kupata maendeleo.

Sauti ya Minja

Minja ameongeza kuwa ili jamii iweze kupata maendeleo ya kweli inapaswa kuchagua viongozi wasiotokana na vitendo vya rushwa na kubadili mitazamo ya kutoa au kupokea rushwa ndio jambo linaweza kukuweka madarakani.

Sauti ya Minja

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wameeleza kuwa rushwa inaweza kusababisha kupata kiongozi ambae sio sahihi na kushindwa kuwaletea maendeleo.

Sauti za wananchi

Kwa mujibu wa utafiti wa TAKUKURU wa mwaka 2024 kuhusu mianya ya rushwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaonyesha katika kila hatua za mchakato wa uchaguzi kunaviashiria na mianya ya rushwa kabla na baada ya uchaguzi.