Mpanda FM

Samia aahidi kuimarisha miundombinu Katavi

18 October 2025, 5:49 pm

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha mapinduzi CCM,Dk Samia Suluhu Hassan.Picha na the Guardian.

kama watampa ridhaa ya kuendelea kuiongoza nchi atahakikisha mkoa wa Katavi unapata kipaumbele katika ujenzi wa barabara na madaraja ili kuunganisha mkoa huo na maeneo jirani ya ndani na nje ya nchi.”

Na Restuta Nyondo

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kuimarisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Azimio halmashauri ya manispaa ya Mpanda amesema kama watampa ridhaa ya kuendelea kuiongoza nchi atahakikisha mkoa wa Katavi unapata kipaumbele katika ujenzi wa barabara na madaraja ili kuunganisha mkoa huo na maeneo jirani ya ndani na nje ya nchi.

Sauti ya mgombea Urais CCM akizungumza

Katika hatua nyingine Dkt. Samia amesema kuwa anatambua juu ya madai ya fidia ya wananchi waliopisha ujenzi wa barabara kwa muda mrefu na kuahidi kuwa ataielekeza wizara ya ujenzi kushughulikia changamoto hiyo.

Sauti ya Dk Samia Suluhu Hassain mgombea Urais CCM

Awali wakiomba kura ,wagombea Ubunge wa Jimbo la Mpanda mjini,Katavi,Nsimbo na Tanganyika wametaja changamoto ambazo watazipa kipaumbele kama vile maji,miundombinu na watumishi.

Sauti za wagombea ubunge

Chama cha Mapinduzi kimeendelea na kampeni za kunadi ilani ya chama hicho ikiwa zimesalia siku 11 kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika October 29 mwaka huu.