Mpanda FM

Zaidi ya wananchi 1000 wajiunga na NSSF Katavi

11 October 2025, 4:50 pm

Baadhi ya wafanyakazi wa NSSF Katavi. Picha na Restuta Nyondo

“Tunashukuru wajasiriamali tumefikiwa na sisi”

Na Restuta Nyondo

Zaidi ya  wananchi 1000 waliojiariji katika shughuli ndogo ndogo  za kiuchumi mkoani Katavi wamejiunga uanachana katika mfuko wa hifadhi ya jamii NSSF kwa mwaka.

Akizungmza na Mpanda radio fm wakati wa ufunguzi wa wiki ya huduma kwa wateja uliofanyika katika ofisi za Nssf meneja wa mkoa Jacob Sulle amesema mfuko huo umeanzisha mfumo wa hifadhi skimu kwaajili ya kusaidia kila mwananchi kujiwekea akiba na kunufaika na mafao kama ilivyo kwa wafanyakazi walioajiriwa.

Sauti ya meneja NSSF

Baadhi ya wananchama waliojiunga kupitia mfumo huo wamesema kuwa wanatarajia kunufaika zaidi na kuendelea kukuza biashara zao kupitia mikopo wanayoweza kupata katika mfuko huo.

Sauti za wanachama

Wiki ya huduma kwa wateja hufanyika kimataifa kila mwaka kuanzia 06 hadi 10 october ambapo kwa mwaka huu kwa upande wa Mfuko wa Nssf  imebeba kauli mbiu isemayo Nssf Kidijitali tumeweza.