Mpanda FM

Masanja aahidi kurasimisha vituo vya bodaboda Mpanda

3 October 2025, 3:11 pm

Mwenyekiti wa CHAUMA Katavi akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Mpanda mjini. Picha na Betord Chove

“Tunakwenda kuwatafutia mahali pa kufanya biashara zenu”

Na Betord Chove

Mgombea wa ubunge kupitia chama cha ukombozi wa umma {CHAUMA} Massanja Musa Katambi amesema atakwenda kurasimisha maeneo ya vituo vya  boda boda ili waweze kumiliki maeneo hayo kwa uhalali wanavoendelea na biashara.

Akizungumza katika mkutano wa  kampeni uliofanyika katika viwanja vya soko la Ilembo kata ya Ilembo  mkoani Katavi  amesema kwa muda mrefu wasafirishaji hao wamekuwa wakisumbuliwa kwa kutokua  na maeneo maalumu nay a kudumu ya biashara hiyo hivyo akipita nafasi ya ubunge atakwenda kumaliza changamoto hiyo.

Sauti ya mgombea ubunge

Kwa upande wao baadhi ya vijana wanaofanya shughuli za usafirishaji wakizungumza mara baada ya kusikiliza sera za mkutano huo hususani urasimishaji wa maeneo yao wamepongeza kwa kutambuliwa kwa changamoto hiyo na wamesema kutatuliwa kwa changamoto hiyo kutaongeza ufanisi katika biashara zao.

Sauti maafisa usafirishaji

Katika hatua nyingine Masanja amesema atakwenda kushughulikia sekta ya elimu, afya. Pamoja na kuhakikisha  watu wenye uhitajimaalumu kama wenye ulemavu na wenye changamoto ya afya ya akili  pamoja na wazee wanapata  makazi na haki zote za msingi.