Mpanda FM

Tesha: Limeni kilimo chenye tija

30 September 2025, 2:25 pm

Afisa kilimo kata ya Makanyagio Philemon Tesha. Picha na Anna Mhina

“Mimi nachukulia kilimo ni ile hatua ya mwisho ya kijana aliyefeli maisha”

Na Anna Mhina

Wakulima mkoani Katavi wametakiwa kuachana na kilimo cha mazoea na badala yake wajikite kulima kilimo chenye tija.

Akizungumza kwenye kipindi cha kilimo biashara cha Mpanda radio FM afisa kilimo wa kata ya Makanyagio Philemon Tesha amesema wananchi wengi hawalimi kilimo chenye tija hali inayopelekea kuonekana kilimo ni kama kazi ya watu masikini.

Sauti ya afisa kilimo

Fredy ni mkulima na mkazi wa kijiji cha Itenka A ambaye ameeleza faida mbalimbali alizozipata kwenye kilimo mbali na kupewa tuzo ya mkulima bora wa mkoa wa Katavi lakini pia amefanikiwa kununua usafiri kupitia kilimo.

Sauti ya mkulima

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda wameeleza namna wanavyoichukulia kazi ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuona ni kazi ya watu wasiosoma huku wakihitaji elimu itolewe ili kuwatoa katika mtazamo huo.

Sauti za wananchi