Mpanda FM

Ubovu wa taa za barabarani Katavi kero kwa madereva

20 September 2025, 4:48 pm

Moja ya taa za barabarani katika halmashauri ya manispaa ya Mpanda. Picha na Sultan Kandulu

“Taa za barabarani kuwa mbovu zinaleta changamoto kwetu sisi watumiaji wa vyombo vya moto”

Na Sultan Kandulu

Watumiaji wa barabara mkoani Katavi wametakiwa kuchukua tahadhari nyakati za usiku wanapokuwa barabarani ili kuepukana na ajari kutokana na baadhi ya miuondombinu ya taa kutowaka wakati wa usiku.

Kwa upande wao baadhi ya watumiaji hao hasa madereva bajaji pamoja na pikipiki wamesema kuwa changamoto  wanazokumbana nazo ni pamoja na ajari za barabarani wakati wa usiku.

Sauti za madereva

Akizungumza kwa njia ya simu meneja wa TANROAD mkoa wa Katavi Mwandisi Martin Mwakabende ameeleza kuwa changamoto ya taa hizo kushindwa kuwaka ni vumbi lililoziba katika paneli za sola hizo na kusema kuwa marekebisho yameanza.

Sauti ya meneja wa TANROAD

Aidha mwandisi Mwakabende amewataka wanufaika wa barabara nyakati za usiku kuongeza umakini pindi wanapokuwa barabarani kwa kipindi hiki ambacho wapo kwenye marekebisho.

Sauti ya meneja wa TANROAD