Mpanda FM

Marufuku magari zaidi ya tani 10 mjini

30 August 2025, 3:30 pm

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph. Picha na Anna Mhina

“Ninachoweza kusema ni kwamba magari yote yenye zaidi ya tani 10”

Na Sultani Kandulu

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusufu amewataka wafanyabiashara kushushia bidhaa zao katika eneo la maridadi ili kuepusha msongamano wa magari kwa maeneo ya soko na maeneo ya ndani ya mji.

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Katavi Jamila Yusufu   ametoa agizo hilo na kueleza kwamba magari yote kuanzia tani 10 yanatakiwa kushusha mizigo katika eneo la maridadi na kutaka agizo hilo litatekelezwa na yeyote atakayekiuka agizo atawajibika kulipa faini ya shillingi laki mbili.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya

Wakizungumza kwenye kikao cha kujadili changamoto baadhi ya wafanyabiashara wameeleza kuwa  changamoto  ya kushushia mizigo mbali na maeneo yao ya biashara inawaongezea  gharama za usafirishaji  mdogo kama bodaboda mikokoteni kupoteza muda, pamoja na kuongezeka kwa wizi na bidhaa zao.

Sauti ya wafanyabiashara

Aidha meneja wa TARURA injinia Kahoza Joseph ameeleza kuwa kuna uwezekano wa kuharibu miundombinu ya barabara na mifereji ya maji andapo magari yenye uzito mkubwa yatashushia mizigo maeneo ya karibu.

Sauti ya meneja TARURA