Mpanda FM
Mpanda FM
20 August 2025, 6:59 pm

Mkaguzi wa polisi Jofrey Chaka. Picha na Anna Mhina
“Hakikisheni vyombo vya usafiri vinakuwa bora”
Na Anna Mhina
Jeshi la polisi mkoani Katavi kupitia kitengo cha usalama barabarani limewataka watumiaji wa barabara kutii sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.
Akizungumza na Mpanda redio FM kwenye kipindi cha kumekucha Tanzania mkaguzi wa polisi Jofrey Chaka amesema mtumiaji wa barabara anapaswa kuhakikisha chombo cha moto kinakuwa bora kabla hakijaingia barabarani ikiwemo ubora wa mataili na honi.
Katika hatua nyingine Chaka amewataka madereva bajaji kuacha tabia ya kusimama maeneo ambayo ni hatari kwa kisingizio cha kupakia abiria.
Hata hivyo amewataka madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda kufuata sheria za usalama barabarani hasa wanapokua wakitumia barabara eneo la taa city Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.