Mpanda FM

Wazazi, walezi waleeni watoto katika maadili

15 August 2025, 5:04 pm

Mkuu wa dawati jinsia na watoto Katavi Judith Mbukwa. Picha na Anna Mhina

“Tutengeneze ukaribu na watoto wetu kutawajengea usalama zaidi”

Na Roda Elias

Wazazi  katika manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametakiwa kuhakikisha wanasimamia ndoto za watoto ili ziweze kutimia.

Hayo yamesemwa na mkaguzi wa polisi Judith Mbukwa ambae pia ni mkuu wa dawati jinsia na watoto mkoa wa Katavi kuwa watoto ili wafikie malengo yao wanapaswa kulelewa katika maadili mema na malezi bora.

Sauti ya Mbukwa

 Mbukwa ameongeza kuwa mtoto hatakiwi kunyimwa adhabu anapokosea bali apatiwe adhabu ambayo inastahili kulingana na umri wake kwa lengo la kumuonya na endapo mzazi anapokiuka haki za mtoto serikali itachukua mkondo wake .

Sauti ya Mbukwa

Kwa upande wao baadhi ya wazazi  na walezi wa manispaa ya Mpanda wamesema kuwa kuwa  karibu na watoto na kuwashirikisha mambo ya Mungu ndio kitu pekee kitakachowalinda watoto na kuwa na maadili mema.

Sauti ya wazazi na walezi