Mpanda FM

Uchafu wa mighahawa kero kwa walaji Katavi

12 August 2025, 1:38 pm

Moja ya mgawaha uliopo mtaa wa Mpanda hotal. Picha na Roda Elias

” Unakula chakula unakaa kidogo unaenda kununua flajiri”

Na Roda Elias

Baadhi ya walaji wa vyakula katika migahawa inayopatikana kata ya Mpanda hotel manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamelalamikia suala la uchafu kwa mama lishe wa migahawa hiyo.

Wakizungumza na Mpanda Radio FM walaji hao wamesema kuwa  wanakumbana na changamoto ya kula chakula kisicho safi hali inayowapelekea kuumwa kwa matumbo.

Sauti ya walaji chakula

Kwa upande wao mama lishe wamekanusha malalamiko hayo huku wakiwaomba walaji pindi wanapoona mapungufu katika migahawa yao basi wawambie ukweli papo hapo.

Sauti ya mama lishe

Kwa upande wake afisa afya wa kata ya Mpanda hotel Mikidadi Ibrahim manispaa ya Mpanda mkoani katavi amesema kuwa  zipo sheria zinazomtaka mama lishe kutoa huduma katika hali ya usafi na endapo atakaidi sheria hiyo atatozwa faini ama kufungiwa  utoaji wa huduma ya chakula

Sauti ya afisa afya

Aidha Mikidadi ametoa wito kwa mama  lishe hao kufuata sheria na taratibu ili kuepukana na faini zisizo za lazima.

Sauti ya afisa afya