Mpanda FM

Madereva bodaboda Mpanda watakiwa kuwa na umoja

6 August 2025, 2:21 pm

Picha ya bodaboda zilizoegeshwa kwenye moja ya kituo. Picha na Roda Elias

“Wenyeviti wa vijiwe watilie mkazo jambo hili”

Na Roda Elias

Madereva pikipiki maarufu kama bodaboda wa  kata ya Mpanda Hotel manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametakiwa kuwa na umoja na mshikamano.

Akizungumza na Mpanda Radio FM  mwenyekiti msaidizi wa kanda ya Mpanda Hotel Steven Nsilya  amesema kuwa idadi ya bodaboda wanaojitoa katika matatizo ya wenzao ni ndogo kwani hakuna ushirikiano.

Sauti ya Steven Nsilya

Aidha  Nsilya amewataka wenyeviti wa kila kijiwe  kuweka mkazo kwa madereva hao  na wakikaidi wenyeviti wa vijiwe watoe taarifa ngazi za juu.

Sauti yaNsilya

Kwa upande wao baadhi ya madereva wa bodaboda wametoa maoni yao juu ya suala  la kutokutoa michango huku wakidai kuwa kukosekana kwa upendo ndio chanzo.

Sauti ya madereva

kwa upande wake mwenyekiti wa madereva bodaboda mkoa wa Katavi Isack Joseph amekiri kutoa wito kwa madereva kusaidizana katika shida na raha ili kuwa na mshikamano.