Mpanda FM

DC Tanganyika akemea ubadhirifu

24 July 2025, 10:47 am

Picha ya pamoja ya viongozi wa mradi, katikati ni mkuu wa wilaya ya Tanganyika. Picha na Anna Millanzi

“Kila fedha inayotengwa kwa miradi imelenga kuimarisha ustawi wa jamii”

Na Anna Millanzi

Katika kuhakikisha usimamizi wa rasilimali za umma na uwajibikaji unaongezeka kwa wananchi na viongozi wilayani Tanganyika  mkuu wa wilaya hiyo amezindua mradi wa raia makini.

Mradi huo wa Raia makini unatekelezwa na taasisi mbili zisizokuwa za kiserikali ikiwemo Tosovic na Tupafo  huku mradi huo ukiwa umekuja kwa dhumuni kuhimarisha uwajibikaji na uwazi kwa wananchi.

Wakizungumza wakati wakiwasilisha risala za taasisi hizo mbili Bwanali Kondowe mkurugenzi kutoka taasisi ya TUPAFO na  George Kasabwe katibu mtendaji TOSOVC ambaye alimwakilisha mkurugenzi wa Taasisi hiyo wameeleza maeneo ambayo mradi huo utatekelezwa.

Sauti za wawakilishi wa taasisi

Mkuu wa wilaya ya Tanganyika akiwa anazindua mradi huo amewasisitiza watumishi wa serikali kusimamia vyema rasilimali za umma ili mthibiti na mkaguzi mkuu wa serikali CAG atakapopita wakati ujao kusiwe na dosari yoyote itakayo jitokeza wilayani humo.

Sauti ya DC

Wadau waliohudhuria katika uzinduzi huo ikiwemo watendaji wa kata ,vijiji pamoja na wenyeviti wa vijiji ambao mradi huo wa raia makini unaokwenda kutekelezwa wameeleza namna ambavyo wamepokea maagizo na kuahidi kuyafanyia kazi.

Sauti za wananchi

Mradi wa Raia makini unaotekelezwa na Taasisi hizo mbili wilayani Tanganyika ni mradi unaotokana na  taasisi ya wajibu wakishirikiana na Policy Forum huku mradi huo ukifadhiliwa na Umoja wa Ulaya