Mpanda FM

Viongozi wa kidini, kimila na wazee maarufu Katavi wanolewa

19 July 2025, 5:36 pm

Stewart Kiyombo Kaimu mkurungezi TAKUKURU Katavi. Picha na Blessing Kikoti

“Wananchi waunge mkono vita dhidi ya rushwa ya kisiasa”

Na Blessing Kikoti

Uwepo wa rushwa katika jamii mkoani Katavi umetajwa kusababisha wananchi kuchagua viongozi wasiostahili na wasiokuwa na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao katika jamii.

Hayo yamebainishwa na kaimu katibu Tawala mkoa wa Katavi Florence Chrisant katika mafunzo yaliyoandaliwa na Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoa wa Katavi Takukuru ambayo yalikuwa yamelenga  viongozi wadini, wakimila na wazee maarufu.

Sauti ya Chrisant

Stewart Kiyombo Kaimu mkurungezi Kutoka taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoa wa Katavi amesema kuwa mapambano ya kuzuia rushwa si kazi ya TAKUKURU pekee bali ni ya jamii nzima hivyo ameiomba jamii kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa juu ya  vitendo hivyo.

Sauti ya Stewart

Kwa upande wao baadhi ya washiriki katika mafunzo hayo wameishukuru TAKLUKURU mkoa wa Katavi kwa kuandaa mafunzo  ambayo yamewapatia elimu  itakayoisaidia jamii katika mapambano dhidi ya rushwa.

Sauti ya washiriki

Taasisi ya kuzuia na kupamba na Rushwa TAKUKURU mkoa wa Katavi imeendesha mafunzo hayo wakati Tanzania ikiendelea kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika October mwaka huu.