Mpanda FM

Wajasiriamali Mpanda wakabidhiwa zaidi ya shilingi million 800

5 July 2025, 4:35 pm

Picha ya wananchi walionufaika wa mkopo wa asilimia 10. Picha na Samwel Mbugi

“Tunamshukuru Rais Samia kwa kuweza kutuona sisi vijana”

Na Samwel Mbugi

Baadhi ya wananchi manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi ambao ni wanufaika wa mkopo wa asilimia 10 wameishukuru serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali na kuwapa mkopo.

Wameyasema hayo wakati wa zoezi la kukabidhiwa Hundi wanufaika ambao ni wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika ukumbi wa manispaa ya Mpanda

Sauti ya wanufaika

Awali akisoma taarifa mbele ya mgeni Rasmi Irene Samson Kileo ambae ni mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii manispaa ya  Mpanda amsema vikundi vilivyokidhi vigezo ni 86 kati ya 126 vitanufaika na mkopo huo ambao ni milioni 839,725,000/=.

Sauti ya afisa maendeleo ya jamii

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ambae alikuwa mgeni rasmi amesema kuwa vikundi ambavyo bado havijapata mkopo visivunjike moyo atahakikisha navyo vinapata kwa awamu nyingine.

Sauti ya mkuu wa wilaya

Jamila ameongeza kuwa mkopo huo ukatumike kama walengwa walivyoomba na kurejesha kwa wakati ili wananchi wengine waweze kunufaika