Mpanda FM

Mfumo dume unaathiri vipi mwanamke kuwania nafasi za uongozi?

1 July 2025, 11:57 am

Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Isinde. Picha na Anna Mhina

“Mfumo dume unaanzia nyumbani hivyo tunakosa kujiamini”

Na Anna Mhina na Roda Elias

Kuendelea kuwepo kwa mfumo dume miongoni mwa baadhi ya jamii kumetajwa kumuathiri mwanamke  katika kuwania nafasi za uongozi.

Wakizungumza na Mpanda FM wakazi wa kijiji cha Isinde kata ya Mtapenda halmashauri ya Nsimbo mkoani Katavi wamesema mfumo dume unamfanya mwananmke kukosa hali ya kujiamini hata katika nafasi za uongozi.