Mpanda FM

Majirani wakerwa na choo cha muuza pombe

30 June 2025, 5:42 pm

Choo kinachowakera ya wananchi. Picha na Anna Mhina

“Hapa sisi tunapata shida na harufu ya kinyesi”

Na Anna Mhina

Baadhi ya wananchi wa kata ya Mpanda hotel manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamelalamikia kero wanayoipata ya harufu mbaya ya choo kilicho karibu na kilabu cha pombe za kienyeji  na jinsi inavyohatarisha afya zao.

Wakizungumza na Mpanda radio FM kwa nyakati tofauti wananchi hao wameongeza kuwa choo hicho cha Jirani yao ambaye ni muuzaji wa pombe za kienyeji kinatoa harufu kali na kipo katika mazingira hatarishi kwao na watoto wao.

Sauti za wananchi

Nae mmiliki wa choo hicho James Christopher amekiri kujua changamoto hiyo na kudai kuwa yupo katika mikakati ya ujenzi wa choo bora.

Sauti ya mmiliki

Ibrahimu Msanda ni mwenyekiti wa kata ya Mpanda hotel amekiri kupokea taarifa hizo za kutokuwepo kwa choo bora na kuwapa muda wapangaji wa eneo hilo hadi pale choo kitakapokamilika.

Sauti ya mwenyekiti

Kwa upande wake afisa afya wa m anispaa ya Mpanda Erick Kisaka amesema kuwa sheria zimewekwa wazi kwa wale ambao wataenda kinyume hatua za kisheria zitachukuliwa.

Sauti ya afisa afya

Mpaka sasa katika kata ya mpanda hotel, jumla ya kaya 40 zimepewa ilani ya onyo ili kuboresha vyoo vya kaya zao kwa lengo la kuepuka kuenea kwa magonjwa ya mlipuko.