Mpanda FM

Wanufaika wa TASAF wammwagia maua Rais Samia

28 June 2025, 5:32 pm

Picha ya pamoja ya viongozi wa serikali na wanufaika wa TASAF. Picha na Samwel Mbugi

“Tupende kuwashukuru viongozi na mama Samia”

Na Samwel Mbugi

Baadhi ya wanufaika wa mfuko wa kaya masikini  TASAF wametoa shukurani kwa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuwajali na kuwezesha  kiuchumi.

Wameyasema hayo wakati  wa kikao cha tathimini ya shughuli za TASAF kwa mwaka wa 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Katavi ambapo wamesema mfuko huo umekuwa mkombozi kwa familia zao.

Sauti ya wananchi

Katibu tawala mkoa wa Katavi Albert Msovela amesema kuwa wataendelea kuwatia moyo wanufaika wa TASAF kupitia msaada unaotolewa na mfuko huo kwa kuwahamasisha kujishughulisha na shughuli mbalimbali ikiwemo ufugaji na kilimo cha bustani.

Sauti ya Msovela

Ikumbukwe kuwa mfuko wa TASAF ni  kuongeza fursa za kujiongezea kipato na kuboresha huduma za kiuchumi na kijamii kwa kaya za walengwa na kulinda maslahi ya watoto wao.