Mpanda FM

Mtoto wa miaka 7 afa maji Katavi

23 June 2025, 12:09 pm

Mto Misunkumilo wananchi wakiendelea na shughuli zao. Picha na Anna Mhina

“Maeneo ya mtoni sio maeneo rafiki kwa watoto”

Na Roda Elias

Mtoto Aliefahamika kwa jina la Barnaba Daniel (7) mkazi wa  kata ya Makanyagio manispaa ya  Mpanda mkoani Katavi amefariki dunia baada ya kuzama mto Misunkumilo.

Tukio hilo limetokea juni 18 /2025 majira ya saa 6 mchana  katika mto misunkumilo eneo la Machinjioni huku chanzo kikidaiwa kuwa mtoto huyo alienda mtoni kwa lengo la kuogelea.

Wakizungumza na Mpanda Radio FM baadhi ya wananchi waliokuwa karibu na tukio hilo wamesema kuwa mtoto huyo ni mgeni katika eneo hilo.

Sauti ya wananchi

Kwa upande wake mjumbe wa mtaa huo Maneno Joseph ameeleza namna ambavyo alipokea taarifa ya tukio hilo ambapo amesema kuwa alipofika eneo la tukio palikuwa na watu wengi huku nguo za mtoto zikiwa chini.

Sauti ya mjumbe

Naye mwenyekiti wa mtaa huo Ibrahim Mzanda amesema kuwa baada ya kupata taarifa hiyo alifika eneo la tukio na kukuta wasamalia wema wameutoa mwili wa mtoto mtoni huku akitoa rai kwa wazazi kuwalinda watoto.

Sauti ya mwenyekiti

Jitihada za kumtafuta kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Katavi David Mutasya zilifanikiwa na kusema kuwa taarifa hizo  bado hazijamfikia ofisini kwake.