Mpanda FM

Zingatieni sheria na miongozo ya uchimbaji-DC Mpanda

13 June 2025, 5:12 pm

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph. Picha na Anna Mhina

“Changamoto zilizopo ni kutokutekelezwa kwa sheria ya usalama mahala pa kazi”

Na Anna Mhina

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph amewataka wachimbaji wa madini kuzingatia sheria na miongozo ya uchimbaji ili kutosababisha madhara yanayoweza kuepukika.

Jamila ameyasema hayo kwenye kikao cha mafunzo ya wachimbaji yaliyofanyika katika ukumbi wa manispaa ya Mpanda na kusema kuwa miongoni mwa changamoto wanazokumbana nazo ni pamoja na kutokutekelezwa kwa sheria ya usalama na afya maeneo ya kazi.

Sauti ya DC Jamila

Kwa upande wake meneja wa mamlaka  ya usalama na afya mahala pa kazi (OSHA) kanda ya nyanda za juu kusini Wilbert Ngowi ameeleza lengo la kuandaa mafunzo hayo kwa wachimbaji ni kuwapa uelewa wa jinsi ya kuboresha mazingira ya kazi.

Sauti ya meneja OSHA

Nao baadhi ya wachimbaji waliohudhuria mafunzo hayo wameeleza namna ambavyo mafunzo hayo yatakavyoleta mabadiliko katika shughuli zao za uchimbaji.

Sauti ya wachimbaji

Zaidi ya wachimbaji wa madini 200 wameshiriki mafunzo hayo yaliyoandaliwa na ofisi ya mkuu wa wilaya ya Mpanda kwa kushirikiana na mamlaka  ya usalama na afya mahala pa kazi (OSHA).