Mpanda FM

Mpanda FM yatoa taulo za kike kwa wanafunzi

11 June 2025, 2:54 pm

Watangazaji wa Mpanda FM wakikabidhi moja ya taulo za kike. Picha na Samwel Mbugi

“Kuna haja ya kukiboresha chumba cha kujistiri kwa mtoto wa kike”

Na Edda Enock

Kuelekea madhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika Mpanda Radio  FM kwa kushirikiana na wadau  mbalimbali wamegawa  taulo za kike kwa wanafunzi wa kike shule ya Rungwa Secondari pamoja na mpanda girls na baadhi ya wanafunzi kutokea shule mbalimbali  mkoani Katavi na kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia.

Meneja  wa Mpanda Radio FM Denis Mkakala amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa kituo hicho kusaidia jamii hasa watoto wa kike kwa kutoa elimu na kuwawezesha kupata vifaa vya kujisitiri wakati wa hedhi.

Sauti ya meneja Mpanda radio FM

Baadhi ya wanafunzi walioshiriki zoezi hilo wamewashukuru Mpanda radio FM kwa kuwagawia taulo za kike huku wakisema kuwa elimu waliyoipata itawasaidia kuwa na ujasiri wa kuripoti matukio ya ukatili na kujitunza  wakati wa hedhi.

Sauti ya wanafunzi

Akizungumza kwa niaba ya mwalimu mkuu wa shule ya Sekondari Rungwa mwalimu Mackson Mapunda  ameipongeza Mpanda radio FM kwa hatua hiyo waliyoifanya huku akisema kuwa ni hatua muhimu ya kuhamasisha usawa wa kijinsia na kuboresha mahudhurio ya wanafunzi wa kike shuleni wanapokuwa katika kipindi cha hedhi.

Sauti ya mwalimu

Utolewaji wa elimu ya ukatili wa kinjia shuleni hapo umefanywa na afisa ustawi wa jamii manispaa ya Mpanda na dawati la jinsia ambapo wamewataka wanafunzi hao kujiamini na kutoa taarifa pale wanapoona   vitendo vya ukatili vikifanyika.