Mpanda FM

Nishati safi fursa kwa mama lishe

26 May 2025, 1:20 pm

Mama lishe wilaya ya Tanganyika baada ya kupokea mitungi ya gesi. Picha na Eda Enock

kumekuwa na ongezeko kubwa la ukataji miti mkoa wa Katavi kwasababu watu wengi hawajafikiwa na nishati safi”

Na Eda Enock

Wananchi mkoa wa Katavi wametakiwa kuepukana na matumizi ya nishati chafu ili kuepukana na hatari zinazoweza kuhatarisha afya na mazingira.

Ameyasema hayo  Mbunge wa viti maalum mkoa wa Katavi Matha festo Maliki  may 18/5/2025 ambapo  ametangaza nia yake ya kuhamasisha kampeni ya Rais  DKT. Samia Suluhu Hassan  kuhusu matumizi ya nishati safi kwa kugawa mitungi ya gesi kwa wajasiliamali wadogo maarufu kama Mama ntilie katika wilaya ya Mpanda na Tanganyika.

Sauti ya mbunge viti maalumu mkoa wa Katavi Martha Maliki

Kwa upande wao wajasiriamali wamemshukuru Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Katavi Matha Maliki kwa kuwapatia mitungi ya Gesi  kwani ni  hatua muhimu katika kuwapunguzia adha ya matumizi ya nishati hatarishi na kuboresha maisha ya wananchi.

Sauti ya mama lishe wilaya ya Mpanda na Tanganyika

Ikumbukwe kuwa hivi karibuni Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan alisema lengo la serikali ifikapo 2034 asilimia 80 ya watanzania watakua wanatumia nishati safi na salama ili kulinda ustawi wa afya za wananchi.