Mpanda FM

 Chatu azuia ufyatuaji tofali kasimba

26 May 2025, 12:42 pm

Picha ya Chatu. Picha na Bertod Chove

Msikitini hapa pana shule ya watoto wadogo ni vema kuchukua tahadhari na kila mtu kuwa mlinzi wa mwenzie”

Na Bertod Chove

Baadhi ya wananchi wanaofanya shughuli za kilimo na ufyatuaji tofali katika moja ya bonde linalopatikana eneo la Kasimba Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wanahofia kuendelea na shughuli hizo mara baada ya kumuona nyoka  aina ya chatu.

Wakizungumza na Mpanda radio fm wananchi hao  wameiomba mamlaka kutatua changamoto hiyo ili waweze kuokoa mazao yao  na kuendelea na shughuli za uzalishaji katika eneo hilo ili kujikimu kiuchumi na kupata chakula kwa ajili ya familia zao.

Sauti ya wanawake wa mtaa wa Kasimba

Kwa upande wake Bernad  Nswima mwenyekiti wa mtaa wa Kasimba amesema katika jitihada za kutokomeza makazi ya nyoka amewataka wananchi ambao ni wamiliki wa viwanja katika eneo hilo kufanya usafi ili kutokomeza makazi ya nyoka hao.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa wa kasimba Bernad Nswima

Ikumbukwe miezi ya hivi Karibuni serikali kwa kushirikiana na wananchi katika eneo hilo walifanikiwa kuwauwa nyoka   wawili aina ya chatu  katika eneo hilo.