Mpanda FM

Madereva wapewe elimu ya kununua mafuta

3 May 2025, 12:56 pm

Picha ya Hassan Masanja mhandishi kitengo cha mafuta kanda ya magharibi. Picha na Anna Mhina.

“Hairuhusiwi kubeba mafuta kwenye madumu”

Na Rhoda Elias

Baadhi ya madereva wa vyombo vya moto  wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi, hawana uelewa wa  kutosha juu ya njia mbadala ya kifaa cha kubeba na kununulia mafuta. 

Wakizungumza na Mpanda Radio FM Madereva hao wamedai kuwa, pindi vyombo vyao vya moto vinapoishiwa mafuta inawalazim kubeba kwenye maduka.

Sauti ya madereva

Hassan Masanja mhandishi kitengo cha mafuta kanda ya magharibi  kutoka mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji (EWURA) amesema kuwa hairuhusiwi kubeba mafuta katika madumu  badala yake ni kutumia vifaa maalumu vya kubebea mafuta.

Sauti ya mhandisi

Mnamo septemba 2024 mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji EWURA iltangaza katazo la kubeba na kuuza  mafuta katika madumu.