Mpanda FM

Wakuu wa shule za msingi Katavi waazimia kupandisha ufaulu

1 May 2025, 1:52 pm

Picha ya wakuu wa shule za msingi Katavi. Picha na Samwel Mbugi.

“Jiwekeeni malengo ili mpandishe ufaulu”

Na Samwel Mbugi

Walimu wakuu wa shule za msingi mkoa wa Katavi wametakiwa kusimamia msingi wa utawala bora na uwajibikaji  katika kazi ili kuleta tija ya ufaulu kwa wanafunzi.

Hayo yamesemwa na katibu tawala mkoa wa Katavi Albert  Msovela ambae alikuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa TAPSHA uliofanyika  shule ya Sekondari Nsimbo ukijumuisha walimu wakuu wa shule za msingi.

Sauti ya katibu tawala

Kwa upande wake afisa elimu mkoa wa Katavi Dafrosa Ndalichako amesema kuwa walimu wanatakiwa kujiwekea malengo na kujitathimini  ili kupandisha matokea ya ufaulu kwa wanafunzi.

Sauti ya Afisa elimu mkoa

Mwenyekiti wa  umoja wa walimu wakuu TAPSHA mkoa wa Katavi Keneth Sichalwe amesema kuwa maagizo yote yaliyoagizwa na katibu tawala wataenda kuyatekeleza na kuinua ufaulu kwa wanafunzi kama ilivyoagizwa.

Sauti ya mwenyekiti wa umoja wa walimu