Mpanda FM

Maafisa uchaguzi Mpanda wapigwa Msasa

30 April 2025, 10:33 am

Picha ya mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Asina Omari. Picha na John Benjamin

“Tekelezeni zoezi hilo kwa umakini”

Na John Benjamin

Maafisa uchaguzi ngazi ya kata wa halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametakiwa kuhakikisha wanasimamia kanuni na sheria katika zoezi la uandikishaji wa daftari la mpiga kura.

Hayo yamebainishwa na mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari katika ufunguzi wa mafunzo kwa maafisa uchaguzi ngazi ya kata manispaa ya Mpanda ambapo  ameleeza kuwa kila mmoja anapaswa kutekeleza zoezi hilo kwa umakini na kuhakikisha hakuna changamoto yoyote inajitokeza.

Sauti ya mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi

 Afisa uchaguzi wa halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi Deudatus Kangu amewataka maafisa uchaguzi kusimamia majukumu yao ya uandikishaji wa daftari la mpiga kura kwa weredi bila ubaguzi wa vyama vya kisiasa, udini wala ukabila

Sauti ya  Afisa uchaguzi wa halmashauri ya manispaa ya Mpanda

Kwa upande wao baadhi ya waandikishaji ngazi ya Kata waliokuwa wakipatiwa mafunzo hayo wameahidi kwenda kutenda haki kwa kusimamia na kutekeleza yale walioyoagizwa na kufundishwa kuhakikisha zoezi hilo linakamilika kwa ufasaha

Sauti ya waandikishaji

Mei mosi kunatarajiwa kuanza zoezi la uandikishaji wa daftari kwa ajili ya mpiga kura kuelekea uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi wa 10 mwaka huu.