Mpanda FM

Namba za NIDA 2019 – 2023 kufutiwa usajili

29 April 2025, 1:12 pm

Picha ya Afisa NIDA Katavi Mauna Karumbeta. Picha na Samwel Mbugi

“Namba zinaenda kufutiwa usajili ni zile  zilizotumiwa ujumbe”

Na Samwel Mbugi

Baadhi ya wananchi mkoani Katavi wametoa maoni mseto kuhusiana na zoezi la kufutiwa usajili wa namba za nida ambazo vitambulisho vilishatoka lakini havijachukuliwa.

Wakizungumza na Mpanda radio FM wamesema kuwa serikali iongeze muda ili wananchi ambao hawana taarifa ziweze kuwafikia na kuchukua vitambulisho vyao.

Sauti ya wananchi

Kwa upande wake afisa wa NIDA mkoa wa Katavi Mauna Karumbeta  amesema kuwa namba ambazo zinaenda kufutiwa usajili ni zile  zilizotumiwa ujumbe kutokana na wahusika kushindwa kuchukua vitambulisho .

Sauti ya Afisa NIDA

Karumbeta ameongeza kuwa vitambulisho hivyo ni vile ambao vilitoka kuanzia mwaka 2019 hadi 2023 na kutokuchukuliwa na wahusika vitahusika katika ufutwaji wa usajili .

Sauti ya Afisa NIDA

Ikumbukwe kuwa ukiwa na namba au kitambulisho cha nida kinakusaidia kupata huduma nyingi za kijamii, kiuchumi na kiusalama.