Mpanda FM

Vijana jitokezeni kugombea nafasi za uongozi

26 March 2025, 3:43 pm

Picha ya mwenyekiti wa ngome ya vijana ACT Katavi. Picha na Anna Mhina

“Taifa linahitaji nguvu kazi ya vijana”

Na John Benjamin

Vijana mkoani Katavi wameombwa kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali  katika uongozi wa kisiasa

Hayo yamezungwa na mwenyekiti wa ngome ya vijana wa chama cha ACT Wazalendo mkoa wa Katavi ambapo amesema kuwa taifa linahitaji nguvu kazi ya vijana na kuwaomba vijana kujitokeza kuwania nafasi mbali mbali bila kujali vyama vyao

Sauti ya mwenyekiti wa vijana

Aidha amesema kuwa chama cha ACT  Wazalendo kinaendelea kujipanga kuhakikisha kinaendelea kutoa nafasi za vijana kujiunga na kuwania nafasi mbali mbali za uongozi kupitia chama hicho

Sauti ya mwenyekiti ACT

Chama cha ACT Wazalendo tarehe Apr 1 mwaka wa huu kinatarajia kufanya uzinduzi wa kampeni yake ya Oparesheni linda Demokrasia kuelekea uchaguzi mkuu.