Mpanda FM

Madereva bajaji wafanya uchaguzi Mpanda

11 March 2025, 4:28 pm

Picha ya madereva bodaboda. Picha na Edda Enock

“Waliochaguliwa watimize ahadi walizotuahidi”

Na Edda Enock

Maafisa usafirishaji bajaji manispaa ya Mpanda mkoani Katavi  wamefanya uchaguzi wa viongozi kwa ngazi mbalimbali.

Akitangaza matokea ya uchaguzi huo mwenyekiti wa uchaguzi huo Mrisho Seleman Ally  amesema kuwa nafasi ya ukatibu Kulikua na wagombea wawili ambao ni Hamidu Selemani ambae amepata kura 31 na Magullat John ambae amepata kura 304, na  kwa upande wa uenyekiti  wagombea walikua wawili ambao ni Aden Sandanda ambae ameibuka na kura 255 na Boniface Mayanga ameibuka na kura178 na kumtangaza Aden Sandanda kuwa mshindi wa uenyekiti wa usafirishaji manispaa ya Mpanda.

Sauti ya mwenyekiti wa uchaguzi

Kwa upande wake mwenyekiti mpya wa usafirishaji bajaji  manispaa ya   Mpanda Aden Sandanda amewashukuru waendesha bajaji kwa kumpatia kura na kauhidi kufanya kazi kwa kushirikiana na waendesha bajaji wote kwa maslahi mapana na kutekeleza yale yote aliyowaahidi.

Sauti ya Sandanda

Boniface Mayanga Ambae ni moja ya wagombea waliokuwa wakigombea nafasi ya uenyekiti wa maafisa usafirishaji amekubaliana na matokea yaliyotangazwa na kusema kuwa uchaguzi ulikuwa wa huru na haki na kueleza kuwa wapo tayari kushirikiana na Washindi hao.

Sauti ya wagombea

Uchaguzi huo umefanyika tarehe 7/3/2025  na matokeo yametangazwa soko kubwa stendi ya bajaji ambapo jumla ya watu waliopiga kura ni 335.