Mpanda FM

Wenyeviti waeleza msaada wanaoutoa mwili wa marehemu ukizuiwa

13 February 2025, 12:02 pm

picha na mwananchi

huwa hawazui miili ya marehemu  bali kuna taratibu za kufuata kutokana na pesa ambazo serikali zimewekeza kwenye sekta ya afya.

Na Lilian Vicent -Katavi

Baadhi ya wenyeviti wa mitaa  mkoani Katavi wameeleza taratibu ambazo wanachukua iwapo ikitokea mwananchi ambaye ameshindwa kuchukua mwili wa marehemu kutokana na kushindwa kumudu gharama zilizotumika kwa ajili ya matibabu.

Wakizungumza na Mpanda Redio FM  wamesema kuwa wao kama viongozi wanaoaminiwa na wananchi wamekuwa wakihusika katika kuthibitisha utambulisho wa watu  hao.

Sauti za wenyeviti wa serikali za mitaa

Akizungumza na Mpanda Radio FM  Mganga mfawidhi wa hospitali ya Rufaa mkoa wa Katavi  Banuba Deogratis amesema kuwa huwa hawazui miili ya marehemu  bali kunataratibu za kufwata kutokana na pesa ambazo serikali zimewekeza kwenye sekta ya afya. 

Sauti ya Mganga mfawidhi wa hospitali ya Rufaa mkoa wa Katavi  Banuba Deogratis

Deogratis ameongeza kuwa  zaidi ya million ishirini mpaka sasa hazijalipwa na watu waliopewa huduma lakini asilimia kubwa wananchi wengi wakishapewa kibali cha kuzika huwa hawalipi fedha hizo.