Mpanda FM

Sungusungu asababisha kifo cha mwananchi

13 February 2025, 11:22 am

picha na mwananchi

amefariki baada ya kupigwa na Sungusungu kwa tuhuma za kushukiwa anajishughulisha na vitendo vya wizi.

Na Betold Chove -Katavi

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika  Onesmo Buswelu amekemea vitendo vya Wananchi kujichukulia sheria mkononi, hali inayopelekea uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya raia wengine.

Buswelu ameyasema hayo katika Kijiji cha Vikonge alipohudhuria mazishi ya Mwananchi Mmoja, aliyefahamika kwa jina la Justine (28), ambaye alifariki baada ya kupigwa na Sungusungu kwa tuhuma za kushukiwa anajishughulisha na vitendo vya wizi.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Tanganyika


Kwa upande wake mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Tanganyika, OCD P. Mashimbi amesisitiza kuwa sheria za nchi haziruhusu Wananchi kujichukulia sheria mkononi.

Sauti ya mkuu wa polisi wilaya ya Tanganyika