Mpanda FM

“Kifo cha Askofu Laban pigo kwa wananchi na serikali”

13 February 2025, 11:09 am

viongozi wa dini,serikali akiwemo mkuu wa mkoa Katavi aliyevaa nguo nyeusi na mtandio mweusi na wageni kutoka nje ya nchi ambao wamehudhuria mazishi

kiongozi huyo ambaye  alikuwa mwalimu wa maadili mema, mshauri wa jamii, na kiongozi aliyekuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo.

Na Anna Mhina -Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko, Ameshiriki  katika mazishi ya Askofu  wa kanisa la New Harvest Church, Dkt. Laban Ndimubenya, February 09 katika kanisa la New Harvest Church, Mikocheni, Manispaa ya Mpanda  mkoani Katavi.

Katika hotuba yake,  Mrindoko ameeleza kuwa kifo cha Askofu Dkt. Laban ni pigo kubwa kwa Taifa, kutokana na umuhimu wa kiongozi huyo ambaye  alikuwa mwalimu wa maadili mema, mshauri wa jamii, na kiongozi aliyekuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo.

Sauti ya mkuu wa mkoa

RC Mrindoko ameongeza kuwa Serikali itaendelea kumuenzi Askofu Dkt. Laban kwa kuthamini mchango wake na kuendeleza juhudi alizozianzisha katika sekta mbalimbali.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini, Sebastian Kapufi, amemuelezea marehemu kama mtu aliyekuwa na maono  kwa jamii na mwenye bidii isiyo na kifani katika kupigania maendeleo ya watu wake.

Sauti ya mbunge jimbo la Mpanda mjini

Mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi wa Serikali, maaskofu kutoka madhehebu mbalimbali ndani na nje ya nchi, pamoja na wananchi mbalimbali wa mkoa wa Katavi.

Sauti ya msoma taarifa