Mpanda FM

Wananchi wataka elimu ya ardhi itolewe

31 January 2025, 7:36 pm

Picha ya mwenyekiti wa baraza  la ardhi na nyumba Katavi Gregory Kalashani. Picha na Anna Mhina.

“Wananchi mkoani Katavi wameomba elimu ya ardhi itolewe zaidi”

Na Liliani Vicent

Baadhi ya wananchi mkoani Katavi wametoa maoni yao kuhusiana na hatua za kuchukuliwa na serikali ili kupunguza migogoro ya ardhi.

Wametoa maoni hayo wakati wakizungumza na Mpanda redio FM ambapo wametaka elimu iendelee kutolewa kwa wananchi.

Sauti ya wananchi

Gregory Kalashani ni mwenyekiti wa baraza  la ardhi na nyumba amesema wananchi wengi wamekuwa hawafuati taratibu za kufungua  kesi ya migogoro ya ardhi kwa kupitia fomu maalumu.

Sauti ya Gregory Kalashani

Wananchi wameshauriwa kufika katika Mahakama na vyombo maaalum vya kutatua migogoro ya ardhi ikiwemo  Baraza la Kijiji la ardhi ,Baraza la kata ,Baraza la ardhi na nyumba la wilaya, mahakama kuu na mahakama ya rufaa ili kupata suluhu ya migogoro ya ardhi.