Mpanda FM

Katavi :Watumiaji wa barabara watakiwa kuzingatia sheria za usalama barabarani

16 December 2024, 12:48 pm

picha na mtandao

Watumiaji wa vyombo vya moto wameahidi kufanyia kazi maelekezo waliopatiwa ili kujilinda

Na John Benjamini -Katavi

Mkoa wa katavi umetajwa kuwa na takwimu chache za ajali  barabarani kwa  kipindi cha miezi sita kwa mwaka 2024.

Hayo yamebainishwa na kamishina wa jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani  makao makuu Ramadhani Ng’anzi wakati akizungumza na madereva wa vyombo vya moto   ambapo amewataka Watumiaji wa barabara mkoa wa Katavi kufuata sheria na kanuni za usalama  barabarani ili kuepusha ajali

Sauti ya kamishina wa jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani  makao makuu Ramadhani Ng’anzi

Kwa upande wao baadhi ya watumiaji wa vyombo vya moto wameahidi kufanyia kazi maelekezo waliopatiwa ili kujilinda na kutoa ushirikiano kwa baadhi ya madereva ambayo watavunja sheria na kanuni wanapokuwa bara barani na kupelekea kusababisha ajali.

Sauti ya watumiaji wa vyombo vya moto

Katika Hatua  nyingine Ng’anzi amewataka watumiaji wa vyombo vya moto kuacha tabia ya kubeba idadi kubwa ya abiria  kinyume  sheria.