Mpanda FM

Wakulima Katavi wahitaji kupimiwa udongo katika mashamba yao

10 October 2024, 5:32 pm

Picha na mtandao

“Baadhi yao wamekuwa wakilima kwa mazoea kwani hawatambui kuwa udongo unahitaji nini wakati wa kilimo”

Na Roda Elias -Katavi

Baadhi ya wakulima  wa kijiji Kamsanga kata ya Mnyagala wilayani  Tanganyika mkoani Katavi wameomba kupimwa kwa udongo wao mashambani kabla ya kuanza kilimo.

Wakulima hao wameainisha kuwa Miongoni mwao wamekuwa wakiweka mbolea awamu moja ama mbili licha ya elimu ya kilimo kuwataka kuweka mbolea shambani kwa awamu tatu.

Wakizungumza na Mpanda Radio FM  wakulima hao wamesema kuwa elimu wanayopatiwa ina faida ingawa baadhi yao wamekuwa wakilima kwa mazoea kwani hawatambui kuwa udongo unahitaji nini wakati wa kilimo

Sauti ya wakulima wakizungumza

Kwa upande wake afisa kilimo mkoa wa katavi amewataka  wakulima ambao bado hawajafikiwa kupimiwa ardhi zao wawe wavumilivu kwani serikali injua nini cha kufanya .

Sauti ya afisa kilimo akitolea ufafanuzi suala hilo