Mpanda FM

Katavi: Vijana watakiwa kuchangamkia fursa katika sekta ya kilimo

24 July 2024, 12:00 pm

Wajumbe wa kikao cha jukwaa la vijana la kilimo katika ukumbi  wa LATCU uliopo manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.picha na Lilian Vicent

wajumbe walioshiriki wamebainisha kuwa kupitia jukwaa hilo wanatarajia vijana wataendea kuhamasika

Naa Lilian Vicent Katavi

Vijana mkoani Katavi wameshauriwa kutumia sekta ya kilimo kama  fursa kupitia  majukwaa ya kilimo  .

Rai hiyo imetolewa na  Faridu Mtiru  Afisa kilimo mkoa wa katavi kwenye kikao cha jukwaa la vijana la kilimo katika ukumbi  wa LATCU uliopo manispaa ya Mpanda mkoani hapa   .

Sauti ya Faridu Mtiru  Afisa kilimo mkoa wa katavi

Katika hatua nyingine Mtiru amesema  kuwa vijana walioshiriki katika kikao hicho wanajihusisha na sekta ya kilimo hivyo watasaidia kuondoa mitazamo hasi iliyopo kwa  baadhi ya vijana  kuhusiana na  sekta ya kilimo.

Sauti ya Faridu Mtiru  Afisa kilimo mkoa wa katavi

Kwa upande wake Afisa maendeleo ya jamii kutoka halmashauri ya wilaya ya mlele pamoja na baadhi ya wajumbe walioshiriki wamebainisha kuwa kupitia jukwaa hilo wanatarajia vijana wataendea kuhamasika kuingia kwenye sekta ya kilimo.

Sauti ya Afisa maendeleo ya jamii kutoka halmashauri ya wilaya ya mlele pamoja na baadhi ya wajumbe walioshiriki

Kikao hicho cha jukwaa la vijana la kilimo kimehudhuriwa na wajumbe ambao ni vijana wanaojihushisha na sekta ya kilimo, maafisa kilimo pamoja na maafisa maendeleo  kutoka halmashauri mbalimbali..