Mpanda FM

Bilioni 67 kuinua uchumi wa mkulima wa tumbaku Katavi

19 July 2024, 12:00 am

Zao la tumbaku likiwa shambani. Picha na mtandao

Uzalishaji wa zao hilo umepanda kutoka kilo milioni 6 hadi kilo milioni 11 ambapo ongezeko hilo limesababishwa na serikali nchini Tanzania kuongeza  kampuni 11  kununua  zao hilo.

Na John Benjamini -Katavi

 Zaidi ya shilingi bilioni 67 zimepatikana kwa wakulima wa zao la tumbaku katika mkoa wa Katavi kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2023/2024.

Mkurungezi Mkuu wa Bodi ya Tumbaku Tanzania Stanley Mnovya amesema  kwa msimu 2023/2024 mkoa wa Katavi uzalishaji wa zao hilo umepanda kutoka kilo milioni 6 hadi kilo milioni 11 ambapo ongezeko hilo limesababishwa na serikali nchini Tanzania kuongeza  kampuni 11  kununua  zao hilo.

Sauti ya Mkurungezi Mkuu wa Bodi ya Tumbaku Tanzania

Kwa upande wa wakulima wa tumbaku mkoani Katavi wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassani kwa kupambana kutafuta masoko ya uhakika na kusimamia ulipwaji wa fedha zao kwa  wakati tofauti na misimu mingine.

Sauti ya wakulima wa tumbaku mkoani Katavi

Katika hatua nyingine Mnovya amesema  katika mapato yaliyopatikana kwa wakulima yameweza kunufaisha halmashauri zote zinazolima zao hilo ambapo  zaidi ya kiasi cha shilingi  bilion 2 kama ushuru zimepatikana.