Mpanda FM

Waendesha bodaboda mkoani Katavi wapaza sauti zao kuhitaji uchaguzi

1 May 2024, 11:25 pm

picha na mtandao

Tunasababishiwa ajali ,tunagongwa na Magari bodaboda tunapigwa ,tunanyanyasika

Na Lilian Vicent -Katavi

Waendesha bodaboda mkoani Katavi Wametaka kufanyika kwa uchaguzi wasafu ya uongozi wa boda boda mkoani hapa kutokana na uongozi uliopo madarakani kushindwa kuwatatulia matatizo yanayowakabili.

Wameyasema  hayo wakati wa  kikao cha kusikiliza kero wanazokumbana nazo madereva bodaboda katika ukumbi wa Polisi Club na kusema kuwa  baadhi yao wamekuwa wakipigwa viboko na askari wa ulinzi shirikishi.

sauti za madereva bodaboda wakizungumza juu ya changamoto wanazopitia

Kwa upande wake  Kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa Kaster Ngonyani amesema amesikiliza kero hizo na atazifanyia utatuzi na kueleza  uchaguzi wa kuchagua  wa viongozi wapya wa bodaboda utafanyika tarehe 01 mwezi wa Sita mwaka huu.

Sauti ya Kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa Kaster Ngonyani akizungumza

Naye mwenyekiti  wa bodaboda mkoani hapa Andrea Mwakalambo  ameeleza  kuwa hajawahi kufuatwa na bodaboda yeyote kudai uchaguzi  na kama wanahitaji hivyo ni vyema kufuata utaratibu.

Sauti ya Mwenyekiti wa bodaboda mkoa wa Katavi