Jamii FM

NERIO Mtwara yamwokoa mtoto akitumikishwa kazi ndani Dsm

30 August 2024, 18:13 pm

Afisa ufuatiliaji Judith Chitanda wa pili kutoka kushoto akiwa na baadhi ya wasaidizi wa msaada wa kisheria pamoja na mama mzazi wa binti aliyeokolewa (wa tatu kutoka kushoto) Picha na Musa Mtepa.

Nashukuru kwa kunikomboa kwani nilikuwa nakutana na changamoto nyingi, nilikuwa nanyimwa chakula, mume wa bosi wangu alikuwa ananisumbua ananitaka kimapenzi kufika hapa salama nashukuru na hapa naungana na mama yangu na sitamuacha tena.

Na Musa Mtepa

Kituo cha Msaada na Usaidizi wa Kisheria (NERIO) Paralegal Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara kimefanikisha kumrudisha binti mwenye umri wa miaka 14 aliyekuwa akitumikishwa kazi za ndani jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia tukio hilo Agosti 29, 2024 afisa tathmini na ufuatilia kutoka NERIO Paralegal Judith Chitanda amesema, mnamo Agosti 27, 2024  walipokea shauri kutoka kwa Bi. Kauri Momadi  mama mzazi wa mtoto huyo  raia na mkazi wa nchi jirani ya Msumbiji akiomba kusaidiwa kuonana na mtoto wake baada ya jitihada za awali alizofanya kugonga mwamba kutoka kwa mwajiri wa binti huyo kwa kudai kuwa kitendo hicho ni kinyume na matakwa ya mkataba waliokubaliana kati ya baba, dalali, mtoto na bosi wa kutoondoka au kusafiri katika eneo hilo ndani ya miezi sita .  

Sauti ya Judith Chitanda afisa tathmini na ufuatiliaji kutoka kituo cha msaada na uasaidizi wa kisheria Manispa ya Mtwara Mikindani

Kwa upande wake Bi Kauri Momadi mama mzazi wa binti huyo ameelezea jinsi alivyopotezana na watoto hao huku akikishukuru kituo cha msaada na usaidizi wa kisheria kwa kumwezesha kuonana na mtoto wake.

Sauti ya Kauri Momadi mama mzazi wa binti aliyeokolewa

Akizungumzia hali ya maisha aliyokutana nayo katika ufanyaji wake wa kazi za ndani, binti huyo amesema amekutana na changamoto nyingi ikiwepo ya kupigwa pamoja na kutakwa kimapenzi na mume wa mwajiri wake.

Sauti ya binti aliyekuwa anafanya kazi za ndani jijini Dar es salaam

Musa Issa (19) mtoto wa kwanza wa Bi Kauri Momadi amesema alipokea simu kutoka kwa mama yake akiwa jijini Dar es Salaam alipokuwa akijitafutia maisha baada ya kuona maisha magumu aliyokuwa anayapitia akiwa kwa baba yake.

Sauti ya Musa Issa mtoto wa kwanza wa Bi Kauri Momadi

Aidha Mzee Issa Mohamedi Namiyuya baba mzazi wa binti uyo amesema kupitia tukio hilo amejifunza juu ya suala la ukatili na ajira kwa watoto kuwa siyo kitu kizuri  huku akishangazwa na taarifa ya kuwa mtoto wake amewahi kukutana na changamoto ya kutakiwa kimapenzi na mume wa bosi wake.

Sauti ya Mzee Issa Namiyuya