Jamii FM

Kaimu balozi wa Marekani nchini Tanzania atembelea Bandari ya Mtwara

30 June 2025, 17:11 pm

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala na kaimu balozi wa Marekani Nchini Tanzania Bw Andrew Lentz wakiwa katika ziara ya kutembelea Bandari ya Mtwara(Picha na Musa Mtepa)

Hii ni ziara ya kaimu balozi wa Marekani nchini Tanzania  katika mkoa wa Mtwara ambapo alifanya mazungumzo na mkuu wa mkoa na kutembelea Bandari ya Mtwara na kujionea inavyofanya kazi

Na Musa Mtepa

Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, leo June 30, 2025 ametembelea mkoa wa Mtwara na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa huo, Kanali Patrick Sawala, pamoja na kutembelea Bandari ya Mtwara katika ziara ya kidiplomasia.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kanali Sawala amesema ujio wa Balozi Lentz unaangazia masuala ya diplomasia ya kiuchumi na fursa za uwekezaji mkoani Mtwara.

Sauti ya Kanali Patrick Sawala mkuu wa mkoa wa Mtwara

Kwa upande wake, Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Mkoa wa Mtwara, Bw. Ferdinand  Nyathi, amesema kuwa ziara hiyo inalenga kubaini maeneo ya ushirikiano baina ya Marekani na Tanzania, hususan katika kuimarisha huduma za bandari.

Sauti ya 1 Ferdinand Nyathi Meneja wa Bandari Mtwara
Meneja wa Bandari ya Mtwara Ferdinand Nyathi akikabidhi picha yenye muonekano wa Bandari ya Mtwara kwa kaimu balozi wa Marekani nchini Tanzania (Picha na Musa Mtepa)

Aidha, Bw. Nyathi ameongeza kuwa ziara hiyo ni ishara njema kwa diplomasia ya uchumi kati ya mataifa haya mawili.

Sauti ya 2 Ferdinand Nyathi Meneja wa Bandari Mtwara

Ziara hii ni sehemu ya juhudi za kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya Marekani na Tanzania, hasa katika maeneo ya kimkakati kama bandari, biashara na uwekezaji.