Jamii FM

Door of Hope Tanzania kutoa huduma ya msaada wa kisheria

28 June 2024, 18:18 pm

Mkurugenzi wa Door of Hope Tanzania Clemence Mwombeki akitoa taarifa ya uzinduzi wa kituo cha msaada wa kisheria kwenye mkutano na waandishi habari uliofanyika leo Juni 28,2024 ofisini kwake (Picha na Musa Mtepa)

Huduma za msaada wa kisheria katika kituo cha msaada wa kisheria cha Door of Hope zitatolewa bure kwa kupitia vigezo kama vya kupitia mawakili waliopo kituonina kupitia kikosi kazi cha jumla ya watu 11

Na Musa Mtepa

Taasisi inayofanyakazi ya utetezi, uwezeshaji na usaidizi wa wanawake na vijana pamoja na kukuza masuala ya upatikanaji wa haki  Door of Hope Tanzania leo Juni 28, 2024 imezindua rasmi huduma za msaada wa kisheria katika kituo cha msaada wa kisheria kilichopo mtaa wa Kiyangu Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara.

Akizungmuza na waandishi wa habari kituoni hapo Mkurugenzi Mtendaji wa Door of Hope Tanzania Clemence Mwombeki amesema kuwa taasisi imekuwa ikitekeleza program na afua  mbalimbali   zinazolenga kulinda, kutetea na kukuza haki za binadamu hususani za makundi ya pembezoni ikiwepo Wazee,vijana ,Watoto ,wanawake na watu wenye ulemavu.

Sauti ya 1 Clemence Mwombeki mkurugenzi mtendaji wa Door of Hope Tanzania
Ofis za kituo cha msaada wa kisheria chini ya Door of Hope Tanzania iliyopo mtaa wa Kiyangu Manispaa ya Mtwara Mikindani(Picha na Musa Mtepa)

Aidha Mwombeki amesema kuwa Pamoja na uwezeshaji unaofanywa kwa makundi mbalimbali  taasisi imebaini kuwa asilimia kubwa ya watanzania hawana uelewa  wa haki zao za kiuchumi,kijamii,kisiasa na kitamaduni hivyo kupelekea wengi wao kutofahamu haki na wajibu hali inayopelekea wanapopatia huduma kwa viongozi wao kudhani wamepewa hisani.

Sauti ya 2 Clemence Mwombeki mkurugenzi mtendaji wa Door of Hope Tanzania

Pia Clemence Mwombeki amesema kwa sasa kituo cha utoaji wa  msaada wa kisheria kitajikita kwenye  maeneo makuu  saba ambayo  mara kwa mara kituo kimekuwa kikipokea kesi kutoka kwa walengwa kama vile  kesi zinazo husu haki za wanawake,Watoto ,Mirathi ,Ardhi, Masuala ya ndoa,Jinai na kesi zinazo husu madai.

Sauti ya 3 Clemence Mwombeki mkurugenzi mtendaji wa Door of Hope Tanzania.