Jamii FM

RC Mtwara, wananchi wafanya usafi

25 May 2024, 15:22 pm

Mkuu wa mkoa wa Mtwara kanali Patrick Sawala akifanya usafi katika eneo la barabara ya Mnarani –Magomeni Manispaa ya Mtwara Mikindani (Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wengi wameonesha kufurahishwa kwa kitendo cha viongozi wa serikali ya mkoa na wilaya ya Mtwara kuungana nao katika zoezi zima la usafi na wengi wao wakisema kuwa watakuwa na mwendelezo wa zoezi hilo majumbani mwao

Na Musa Mtepa

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala leo tarehe 25/5/2024 ameongoza Wananchi  wa Manispaa ya Mtwara Mikindani katika zoezi la  usafi lililofanyika katika Barabara ya Mnarani –Magomeni na eneo la makaburi msafa.

Aidha zoezi hilo lililotanguliwa na matembezi ya mwendo wa pole (Jogging) iliyoanzia  katika ofisi za mkuu wa mkoa kuelekea Parishi,Bandarini ,Soko kuu hadi viwanja vya sabasaba ambapo akiwa katika viwanja hivyo amewapongeza Wananchi kwa kujitokeza kwa uwingi huku akiwa na matarajio ya kuwa  zoezi hilo litakuwa endelevu kwa kila inapofika jumamosi ya mwisho ya kila Mwezi.

Sauti ya 1 Kanali Patrick Sawala Mkuu wa mkoa wa Mtwara

Pia Mkuu wa mkoa Kanali Patrick  Sawala ametumia nafasi hiyo kuwaomba Wananchi kuendelea kutunza amani iliyopo na kuvipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuendelea kuifanya Mtwara na Tanazania kuwa salama.

Mkuu wa mkoa wa Mtwara kanali Patrick Sawala ,mkuu wa wilaya ya Mtwara Mwanahamisi Munkunda na Mh.Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Shadida Ndile wakiwa katika matembezi ya Mwendo pole (Picha na Musa Mtepa)
Sauti ya 2 Kanali Patrick Sawala mkuu wa mkoa wa Mtwara

 Nao baadhi ya Wananchi waliojitokeza katika zoezi la usafi wameonesha kufurahishwa na kumpongeza mkuu wa mkoa kwa kitendo hicho cha kuwakutanisha na kufanya usafi Pamoja huku wengine wakisema kuwa zoezi hilo liwe endelevu kama linavyofanyika katika mikoa mingine.

Vikosi vya ulinzi na usalama vikishiriki zoezi la matembezi ya mwendo wa pole na usafi uliofanyika katika viwanja vya sabasaba,makaburi msafa pamoja na barabara ya mnarani –Magomeni(Picha na Musa Mtepa)
Sauti ya baadhi ya wananchi waliojitokeza katika zoezi la usafi hii leo.
Viongozi wa serikali ,vyama vya Siasa na Wananchi wakifanya mazoezi ya kuweka mwili sawa baada ya kukamilika zoezi la matembezi ya mwendo pole(Picha na Musa Mtepa)

Zoezi la usafi lililotanguliwa na matembezi ya mwendo wa pole yamehusisha wananchi,viongozi wa Serikali na vyama vya siasa Pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo ndani ya Manispaa ya Mtwara Mikindani